Idara ya usalama imefungua rasmi kituo cha polisi eneo la Mjambere huko Kisauni kaunti ya Mombasa.
Akizungumza na wanahabari baada ya kufungua kituo hicho mapema hii leo kamishana kaunti ya Mombasa Evans Achoki amesema kituo hicho kitasaidia pakubwa kuimarisha usalama katika eneo bunge la kisauni.
Achoki amesema mikakati imeekezwa kukabili magenge ya wahalifu yanayoangaisha wakaazi wa kisauni na kaunti ya Mombasa kwa jumla.